![]() |
Vicky Ntetema mwandishi mahiri wa Idhaa ya Kiswahili ya Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC). |
Na Frank Bruno.
Tanzania tumejaliwa kuwa na vyombo vya habari vingi
sana nikimaanisha Redio, Runinga pamoja na magazeti. Moja ya sehemu inayo
sisitizwa kwa watangazaji na waandishi kuwa na mtindo binafsi wa kutangaza ni
kwenye somo la uandishi wa utangazaji (broadcast journalism), kwa kurejea vyuo
mbalimbali vya uandishi wa habari kwa mfano Chuo cha Uandishi wa Habari
Morogoro kitengo hiki kipo chini ya Mwezeshaji Ndg Hashim Gulana. Somo ambalo
wanafunzi wengi wa uandishi wahabari, wanalipendelea zaidi kuliko masomo
mengine, wapo ambao mara ya kwanza walipo wasili tu chuoni hapo, karibu
wanafunzi wengi walionesha kupendelea zaidi somo la utangazaji tu bila masomo
mengine.
![]() | |||||||
Baraka wa Kitenge akipewa maelekezo na mtangazaji mkongwe Charles Hillary jinsi wanavyotayarisha habari zao BBC alipotembelea ofisi za BBC. |
Utafiti umebaini, wanafunzi wengi, wanapendelea
sauti zao zisikike zaidi kwa wasikilizaji. Pia wengi wao wanataka wajulikane na
wawe maarufu kama watangazaji wa redio ambazo zilitangulia kurusha matangazo
yake, na karibu wote wanatamani wakafanye kazi katika mkoa wa Dar es salaam
ambako kuna idadi kubwa ya vyombo vya habari.
Tunapo angalia redio na madhumuni yake tunaona
ni chombo kinacholusha matangazo yake ili kuwasiliana na watu, kwa kuburudisha,
kuhabarisha na kufundisha mambo mbalimbali.
Kwa kutaja machache redio za sasa zipo kwa ajili ya maongezi sana maarufu kama
‘Zogo’, ambapo kwa sasa ukitaka uajiliwe redioni unaulizwa una ‘zogo’? Yani una
mudu kuongea sana? Huu ni mtindo mpya unao shika kasi katika redio zetu. Tatizo
lililopo, baadhi ya waandishi wakikosa cha kuongea, hudhubutu hata kuongea
matusi, na kubadilisha studio kua kijiwe cha kusutana.
Kama mtangazaji ni vema ukaingia na muongozo
(script) ambao itakusaidia kukuongoza na kutoongea vitu visivyo hitajika kwa
wasikilizaji. Wasikilizaji wana hitaji kujifunza mambo mengi na changamoto
kupitia vyombo vya habari. Lakini kutokana na uvivu wa baadhi ya waandishi hapa
nchini wa kutofuatilia mambo yanayoibuka kila wakati duniani unatufanya tuingie
kazini kwa kukosa cha kuongea na matokeo yake kuanza kuendesha vipindi vya
udaku.
Osea Mchopa mwanafunzi wa ngazi ya stashaada
katika chuo cha uandishi wa habari morogoro anasema wanachuo wengi katika vyuo
vya uandishi wa habari wanatabia ya kuiga sauti za watangazaji wengine sio
uhalisia wao na ndio maana wanashindwa kuwa wabunifu. “ukifuata misingi
uliyofundishwa ndio kigezo tosha cha kukufanya uweze kufanikiwa” aliongeza
Mchopa.
Pia
Paskalina Kidyara makamu wa rais serikali ya wanafunzi katika chuo cha uandishi
wa habari Morogoro aliongeza kwa kusema kuwa lazima waandishi wawe wabunifu
ingawa tunaweza kuiga namna ya utangazaji lakini sio sauti.
“Haikatazwi kuwa na mtu wako anaekuvutia (role mode) katika utangazaji ila jambo la msingi lazima uwe wapekee katika utangazaji”
alisema Hashim Gulana mkufunzi katika chuo cha uandishi wa habari morogoro
Tunawaona waandishi wakongwe kama Tido Muhando,
George Njogopa, Vicky Mtetema, kwa hao wachache na wengine wengi, walikuwa wanafanya
vipindi makini vilivyo waletea maendeleo makubwa, mpaka kufanya kazi katika
vyombo vya habari maarufu duniani kama BBC & DW.
Tuking'ang'ania kufuata aina fulani ya
utangazaji wa watangazaji wetu wa kisasa hapa nchini hakika hatuwezi kuimalisha
misingi ya utangazaji yenye radha na utamaduni wa kitanzania kama ilivyokua
hapo zamani enzi za kina Charles Hillaly, Julius Nyaisanga, Harima kiemba,
Karim Besta na wengine wengi.
Waandishi wengi huujisahau na mara tu
wanapomaliza masomo yao na kuanza na kuingia rasmi kwenye tathnia ya utangazaji
huegemea zaidi kwenye upande wa burudani hasa ya muziki maarufu kama bongo
fleva. Hakuna mitaala inayo fundisha waandishi waende wakapige miziki, ingawa
kuburudisha ni sehemu ya wajibu wa redio. Kuna habari nyingi sana vijijini na sehemu mbalimbali tunaweza
kutengeneza habari ambazo zina tija ndani ya jamii kuliko burudani.
Tasinia ya habari inalenga zaidi katika
kuinufaisha jamii yake katika nyanja mbalimbali za kimaisha, kwa kutegemea
waandishi walio wabunifu na wenye kujitoa zaidi kwa jamii.
0 comments:
Post a Comment