Habari Mpya

Sunday, February 21, 2016

Takriban Watu 140 wauawa Syria




Takriban watu 140 wameuawa kwa milipuko ya mabomu katika miji ya Homs na Damascus nchini Syria, waangalizi na vyombo vya habari vya serikali vimeeleza.

Takriban milipuko minne ilitokea katika eneo la Sayyida Zeinab mjini Damascus na kuua takriban watu 83. Awali mjini Homs Watu 57 wengi wao raia waliuawa kwa mashambulizi ya mabomu yaliyokuwa yametegwa kwenye magari mawili.

Wanamgambo wa Islamic State wamekiri kutekeleza mashambulizi hayo katika miji hiyo miwili.
Wakati huo huo, Waziri wa mashauri ya kigeni wa Marekani, John Kerry amesema makubaliano ya muda yamefikiwa kati Marekani na Urusi kuhusu suluhu ya mgogoro wa Syria.

  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 comments:

Item Reviewed: Takriban Watu 140 wauawa Syria Description: Rating: 5 Reviewed By: Unknown
Scroll to Top