Kikundi cha The Loyalmedia.blogspot.com kutoka chuo kikuu cha Mzumbe wametembelea chuo cha
Uandishi wa Habari Morogoro MSJ kwa lengo la kujifunza mambo mbalimbali
yanayohusu tasnia ya habari.
Akitoa maelezo katika
chumba cha mikutano chuoni hapo raisi wa serikali ya wanafunzi MSJ MOSJOSO
Kelvin philipo amesema kuwa amefurahishwa na ugeni huo kwani ushirikiano ambao
ulikuwa ukifikiriwa kwa maneno na umeanza kwa vitendo.
“niseme nimefurahishwa
sana na ujio wenu kutokana na mara kwa mara kutafakari juu ya ushirikiano wetu
na Mzumbe kwani sisi tunaonekana kujifunza vitu tofauti hivyo niseme
nafurahishwa sana na haya ninayoyaona kwa sasa hivyo karibuni sana’. Alisema
Kelvin.
Naye waziri wa habari
chuoni hapo Timotheo Lupembe amesema kuwa wanajivunia kuona mzumbe wamewapa
kipaumbele kuja kujifunza masuala ya habari kitu ambacho kitawafanya waungane
kwa pamoja katika kujenga nchi yetu.
Kikundi hiko
kinajihusisha na utoaji wa habari kwa njia mtandao wa kijamii blogs kinahusika
kusambaza picha na habari zinazohusu chuo cha Mzumbe ili kuwahabarisha na
kuwaburudisha wasomaji wao.

0 comments:
Post a Comment