Habari Mpya

Sunday, December 22, 2013

PRESENTATION YA DJ-10, KUHUSIANA NA PRESS COMFERNCE, ILIYOFANYIKA CHUO CHA MSJ, Tarehe 20/12/2013, NA HIVI NDIVYO ILIVYOKUWA........


DAWA MPYA YA KUTIBU MAJI MACHAFU YAGUNDULIKA :
Edited by Godfrey Mgallah.
Kampuni ya Warioba Sanitation inayoshughulika na uchunguzi wa dawa za kutibu maji Mkoani Morogogo yagundua dawa mpya ya kutibu maji machafu.
Dawa hiyo inayotambulika kwa jina la MSELE WATER GUARD ambayo imedhibitiswa na mkemia mkuu wa kampuni hiyo Warioba Igombe na kusema “Dawa hii inauwezo wa kutibu maji machafu ambayo yatakuwa yana rangi mbalimbali na kusababisha kuwa meupe kwa muda mfupi”
Aidha mkemia huyo ameongeza kwa kusema kuwa dawa hiyo imetengenezwa kwa majani ya miti na miziziz katika majaribio ya kamaabara dawa hiyo ina nguvu ya kuuwa bacteria kwenye maji bila kuchanganya kitu chochote.
Hata hivyo mkemia ameongeza na kusema dawa hii nimaarumu kwa mikoa yenye ukame kwani hutumia maji yaliyo kwenye madimwi, mabwawa hivyo basi dawa hii itawasaidia katika usafishaji wa maji yao.  
END
KOZI FUPI YA UTANGAZAJI YAANZISWA:
Edited by Nasibu Babisha.
Chuo Cha Uandishi wa Habari Morogoro (MSJ) kimetangaza kozi mpya ya utangazaji wa Tv na Radio chuoni hapo.
Akiongea na MOSJOSO blog msemaji mkuu wa chuo hicho Michael Sikapundwa amesema kuwa kozi hiyo itaanza mwezi wa kwanza mwaka kesho.
Msemaji huyo aliongeza kwa kusema kuwa kozi hiyo itachukua muda wa mwezi sita kwa gharama ya shilingi laki nne kwa kozi hiyo.
Hatahivyo Mratibu wa mafunzo wa Chuo Cha Uandishi wa Habari Morogoro Godfley Marusu ameongeza kwa kusema “wazo la kuongeza kozi hiyo katika Chuo hicho ni ni kuongeza wataaramu katika tasnia ya uandishi wa habari kwani kuna upungufu mkubwa katika taaluma hiyo”.
END
MZALENDO COMPANY YAANZISHA KOZI MPYA YA KOMPUTA:



Edited by Godfrey Mgallah.
Kampuni ya Mzalendo iliyopo Kihonda Mkoani Morogoro Imetangaza kozi mpya ya Adobe Page Maker ambayo inahusika na utengenezaji wa vitabu, magazeti, majarida, vipeperushi na hata kadi za mialiko.
Akizungumza na MOSJOSO blog Msemaji Mkuu wa kampuni hiyo Frank Bruno amesema kuwa “kozi hii mpya itasomwa kwa miezi mitatu na kuhitimu”.
Aidha aliongeza kwa kusema “kozi hii itamuwazesha mwanafunzi kuajiriwa au kujiajili mwenyewe ili kuendana na soko la ajira nchini”.
Hatahivyo msemaji huyo aliongeza kwa kusema kuwa “mwanafunzi atakaye hitaji kusoma kozi hii atapata fursa ya kusoma bure kozi ya awali ya komputa (introduction of computer).
END
BIDHAA MPYA YA MAZIWA FRESH YAZINDULIWA MOROGORO:


Edited by nasibu babisha.
Kampuni inayojishughulisha na usindikaji wa maziwa ya Jogosha Milk ya mkoa morogoro imezindua bidhaa yake mpya yenye ujazo wa mililita 300 inayofamika kwa jina la Jogosha Fresh Milk.
Akizungumza na MOSJOSO blog msemaji mkuu wa kampuni hiyo Godfrey Mgallah amesema “bidhaa yetu mpya itasaidia kuimarisha mifupa, ngozi na kupunguza kiasi cha sukari mwilini kwa watumiaji wa bidhaa zetu”.
Hatahivyo msemaji huyo ameongeza kwa kusema Jogoha Fresh Milk inapatikana kwa bei za rejareja na jumla katika matawi yake yote ya Iringa, Pwani,Dodoma na Morogoro kwa shilling 500Tsh kwa chupa na katoni moja kwa shilingi 5400.
END
TROPICAL FRESH JNUICE YAZINDULIWA RASMI:

Edited by Godfrey Mgallah.
Kampuni ya Mambo Fresh inayojishughulisha na utengenezaji na usambazaji wa vimiminika vya aina mbalimbali inayopatikana Morogoro Mjini Mkabala na KCB Bank imezindua rasmi kinywaji aina ya TROPICAL FRESH JUICE chenye ujazo wa 500ml na 300ml abayo ni mchanganyiko wa Embe na Apple  .
Akizungumza na MOSJOSO blog msemaji mkuu wa kampuni hiyo Hadija Said amesema kuwa “mbali na Tropical Fresh Juice kuwa na ladha nzuri na yenye kumtamanisha mtumiaji kuitumia wakati wote pia inampatia mtumiaji vitamin C pamoja na kumpa nguvu pindi anapotumia Juice hiyo”.
Hatahivyo msemaji huyo aliongeza kwa kusema bidhaa hiyo ya Tropical Fresh Juice inapatikana kwa jumla na rejareja kwa matawi yote ya kampuni ya Mambo Fresh Company kwa shilling 700/= kwa rejareja na shillingi 6500/= kwa jumla.
END
JUICE YENYE TIBA YAGUNDULIKA:

Edited by Nasibu Babisha.
ALOSERA ni juice inayotengenezwa na kampuni ya CRA iliyopo Manispaa ya Morogoro juice hii imedhibitiswa rasmi na mkemia mkuu wa kampuni hiyo .
Akizungumza na MOSJOSO blog mkemia mkuu wa kampuni ya CRA Robert Mauya amesema kuwa juice hiyo itakuwa na uwezo wa kutibu ugonjwa wa kisukari, kifua kikuu na kuongeza CD4 kwa waadhilika wa ugonjwa wa ukimwi.
Aidha mkemia huyo ameongeza kwa kusema  kuwa “juice hii sio tu inatibu magonjwa bali upunguza kitambi, kuongeza damu na kuongeza vitamin C na D mwilini.
END
  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 comments:

Item Reviewed: PRESENTATION YA DJ-10, KUHUSIANA NA PRESS COMFERNCE, ILIYOFANYIKA CHUO CHA MSJ, Tarehe 20/12/2013, NA HIVI NDIVYO ILIVYOKUWA........ Description: Rating: 5 Reviewed By: Unknown
Scroll to Top