Na Claudia Kayombo
Wanahabari wa Jumuia ya Afrika Mashariki, wanaungana na wenzao duniani kuadhimisha siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari.
Miongoni mwa mambo ambayo yanatarajiwa kutawala wakati wa maadhimisho
hayo ya siku tatu, ni majadiliano ya namna ya kuondoa utata wa
mazingira ya waandishi wa habari kufanyia kazi hususan nchini Tanzania.
Maadhimisho hayo kwa ukanda huo, yanaadhimishwa mkoani Arusha Tanzania.
Hata hivyo wakati katika Jumuia ya Afrika Mashariki wawakishi
wakikutana Arusha, kwa upande wao waandishi wengine wanayaadhimisha kwa
kila mkoa kupitia klabu zao.
Wakati maadhimisho hayo yakifanyika, vichwa vya wanahabari nchini,
vimebeba wasiwasi baada ya
miaka ya hivi karibuni kutokea matukio
yanayotishia usalama wa maisha yao.
Mashaka katika vichwa vya waandishi yamekuja baada ya matukio mawili
ya vifo vya waandishi na la tatu la kutekwa, kung’olewa jicho, meno kwa
mmoja wa nguli wa tasnia hiyo, Absalom Kibanda.
Katika mazingira yanayoonesha kuwa, Kibanda pengine aliponzwa na
ukali wa kalamu yake, ni pale aliposubiriwa katika geti la nyumba yake
na kufanyiwa unyama huo.
Ukweli wa mambo ni kwamba maadhimisho ya siku ya Uhuru wa Vyombo vya
habari duniani yawe mwanzo wa kukoma kwa vitendo vya ukatili dhidi ya
wanahabari nchini.
Pia iwe chachu kwa wamiliki wa vyombo vya habari kuwalipa waandishi
wa habari mishara yao kwa wakati kwani hiyo ni changamoto ambayo sasa
ipo katika ofisi nyingi za vyombo vya habari hivyo kuwafanya wageuke
kuwa ombaomba au wasaliti wa fani hiyo
chanzo na Jambo Leo.

0 comments:
Post a Comment