Habari Mpya

Wednesday, April 17, 2013

KUELEKEA MEI 3 Uhuru Wa Vyombo Vya Habari Utazamwe Upya

Neno ‘uhuru’ linamaanisha ni hali ya kujitawala na kujiamulia kupanga na kutekeleza katika hali isiyo na shuruti pasipo kuvunja sheria na kanuni.
Tarehe 3 mei ya kila mwaka ni siku ya uhuru wa vyombo vya habari Duniani. Kama ilivyo ada mwaka huu pia Tuzo hizo za Umahiri wa Uandishi wa Habari Tanzania (EJAT) ziliandaliwa na Baraza la Habari Tanzania (MCT) na kutolewa katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam juzi. Waandishi wengi waliibuka na tuzo hizo. Kwangu ninazichukulia tuzo hizo kuwa ni changamoto kubwa kwa waliozipata na wasiozipata. Kwa waliopata tuzo tuzo hizo wasibweteke kwa kuwa wametuzwa bali watambue umuhimu wao katika kusaidia jamii katika kuibua kero mbali mbali katika jamii yetu ambazo ni kiwazo cha maendeleo.
Kwa waandishi ambao hawakupata tuzo ni budi wakaongeza bidii katika kuandika habari zenye msukumo wa maendeleo na zenye tija kwa jamii. Japo habari za kijamii ambazo zinaibua kero muhimu katika jamii nyingi kati ya hizo hupatikana vijijini ambako vyombo vyetu vingi vya habari situ havifiki huko bali vyombo vya habari huwa haviwawezeshi waandishi kwenda vijijini kufanya tafiti na kuibuka na habari hizo
Lakini pia ifahamike kuwa kutokana na matakwa na maelekezo ya wamiliki walio wengi habari za kijamii hazina nafasi na haziuzi.Wamiliki wa vyombo vingi vya habari huegemea na kutoa maelekezo kwa wahahariri kuandika habari za kisiasa kwani ndizo huonekena kuwa zina soko na faida nyinginezo hasa mahusiano kati ya wamiliki na watawala.

Ni kawaida yangu kutafakari kwa kina masuala mbali mbali ya kisiasa na kijamii . Nimejijengea mazoea ya kuzama kwa kina kuangalia changamoto mbali mbali zinazokabili jamii ya Kitanzania, Afrika na Ulimwengu kwa ujumla. Kutokana na mazoea hayo ndipo ninapojikuta ninatafakar kwa kina juu ya siku hii adhimu kwa waandishi wa habari. Siku ya uhuru wa vyombo vya habari.

Kama jina la siku linavyojieleza, ‘siku ya uhuru wa vyombo vya habari’. Kabla ya kwenda mbali zaidi yapo maswali ya kujiuliza. Ni uhuru wa vyombo vya habari au uhuru wa waandishi wa habari? Na je chombo cha habari chaweza kuhesabika kuwa huru pasipo mwandishi kuwa huru? Kulingana na hali ilivyo hususani hapa kwetu Tanzania ni yupi mwandishi/ chombo kilicho huru? Na mwisho tujiulize swali hili ni uhuru wa waandishi wa habari/vyombo vy habari au wamiliki wa vyombo hivyo na maswahiba zao wanasiasa?
Hapa kwetu Tanzania tunavyo vyombo vingi sana vya habari. Je viko huru? Tunavitambuaje vyombo vya habari vilivyo huru? Na kwa uapnde wa waandishi wa habari, je ni changamoto zipi zinazowakabili? Wanafanya nini kuzitatua? Hawajafungwa katika minyororo ya dhuruma na manyanyaso ya wamiliki na wanasiasa? Hii ni mada ndefu. Nionavyo ni kama vile uhuru kama wa waandishi waa habari haujapatikana. Uhuru uliopo ambao unahesabiwa kuwa ni uhuru wa vyombo vya habari upo kwa wamiliki wa vyombo vya habari. Kwani hawa wengi wao huamua nini kiandikwe/kitangazwe katika vyombo vyao hususani vyombo vinavyomilikiwa na watu bianafsi.
Kwa upande wa vyombo vinavyomilikiwa na Serikali matakwa ya Serikali (watawala) ndio hutawala katika uendeshwaji wa vyombo hivi. Ijapokuwa vyombo hivi vya serikali huendeshwa na kodi za wananchi lakini hugeuka kuwa vyombo vya propaganda vya serikali. Na tujiulize ni mara ngapi vyombo hivi vya umma vimekejeli vyama vya siasa? Je ni mara gapi vyombo hivi vya umma vimelalamikiwa kupendelea chama tawala hususani wakati wa uchaguzi?

Vyombo vya habari vya binafsi na vya serikali mara nyingi vimelaumiwa kwa kuendesha propaganda zisizo na tija kwa lengo la kumneemesha mtu au kundi fulani.
Sisi waaandishi wa habari wengi wetu tumeacha taaluma zetu zinazoelekeza miiko ya uandishi wa habari. Tumekubali kutumiwa mithiri ya kwa muda mfupi na watu binafsi,wanasiasa na makundi mengene ya kijamii kwa binafsi na kasha kuachwa/kutupwa mithili ya kondom ilikwisha tumika. Licha ya umuhimu mkubwa wa waandishi wa habari katika kufanikisha kampeni za kijamaii lakini mchango wao hauthaminiki sit u na watawala bali hata jamii kwa ujumla wake.
Wamiliki wa Vyombo vya habari wamekuwa ni miungu watu. Manyanyaso visa na mikasa ni sehemu ya adha azipatizo mwandishi wa habari wa Tanzania.

Licha ya waandishi kulipwa ujira mdogo mno usiokidhi mahitaji vyombo vingi vya habari haviwalipi waandishi kwa wakati. Mishahara yao imekuwa ikichelewa mno na kuna wakati hawalipwi kabisa. Hii huwapelekea waandishi kuishi kwa bahati nasibu. Hapo ndipo umahiri wa kazi hupungua na ndipo mwandishi huacha kufuata miiko ya uandishi wa habari na kujitumbukiza katika vitendo vya rushwa na aina nyingine ya ufisadi.
Maisha ya mwandishi wa Tanzania anayeadhimisha uhuru wake ifikapo tarehe 3 may ya kila mwaka yapo mashakani.

Waandishi wengi wanaishi kama omba omba. Kwenye mikutano ya waandishi wa Habari (Press Comference) ni eneo ambalo waandishi huadhirika na kudharirika. Bahasha ndio mkombozi wao
. Baadhi ya waandaaji wa mikutano hii huwanyanyasa waandishi mithiri ya watumwa. Kazi bado na safari ya uhuru kamili ya uandishi ni ndefu. Sheria ya habari ya mwaka 1976 ni kikwazo kingine kwa uhuru kamaili wa uandishi wa Habari na vyombo vya habari. Kuna kila sababu ya kuitazama upya sheria hii. Wamiliki wa vyombo vya habari na wanasiasa ni kiwazo kikubwa kwa uhuru wa waandishi wa habari na ustawi wa taaluma ya uandishi wa Habari Tanzania. Mwisho nimalize kwa kutoa waito kuwa ni vema uhuru wa vyombo vya habari ukatazamwa upya kulingana na changamoto zinazokabili tansinia ya habari Tanzania.
  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 comments:

Item Reviewed: KUELEKEA MEI 3 Uhuru Wa Vyombo Vya Habari Utazamwe Upya Description: Rating: 5 Reviewed By: Unknown
Scroll to Top